Kiungo kutoka nchini Hispania, Cesc Fabregas pamoja na beki wa
pembeni kutoka nchini Brazil Filipe Luis wameanika picha za wachezaji wenzao wa
klabu ya Chelsea katika mtandao wa kijamii wa Instagram kwa dhamira ya
kuonyesha namna walivyokuwa na furaha mara baada ya kupata point tatu ugenini
usiku wa kuamkia hii leo huko mjini Lisbon nchini Ureno.
Fabregas na Filipe Luis, walikuwa sehemu ya kikosi cha Chelsea
kilichoibuka na ushindi katika mchezo huo dhidi ya Sporting Lisbon, wameweka
picha katika mtandao huo zikionyesha matukio tofauti ya furaha.
Picha ya Filipe Luis inaonyesha furaha iliyokuwa imekithiri
miongoni mwa wachezaji wa Chelsea walipokuwa katika vyumba vya kubadilishia na
picha ya Fabregas inaonyesha wachezaji wa Chelsea kwenye ndege tayari kwa
safari ya kurejea jijini London nchini Uingereza.
Katika mchezo huo Chelsea walifanikiwa kuchomoza na ushindi wa
bao moja kwa sifuri lililofungwa na kiungo kutoka nchini Serbia, Nemanja Matic.









No comments:
Post a Comment