Wednesday, October 15, 2014

Cristiano Ronaldo awa staa wa pili kufikisha likes milioni 100 Facebook baada ya Shakira.

10334368_814560345274579_6152529128868119107_n
Mchezaji wa Real Madrid na Ureno, Cristiano Ronaldo amekuwa staa wa pili duniani baada ya Shakira kufikisha likes milioni 100 kwenye mtandao wa Facebook.
Ronaldo pia ni miongoni mwa wanamichezo mwenye followers wengi kwenye mtandao wa Twitter akiwa na milioni 30. Hii ni moja ya sababu inayomfanya mwanamichezo huyo kuingiza fedha nyingi zaidi kuliko wenzie hasa kwenye soka.
Kupitia ukurasa wake wa Facebook wa mwanamichezo huyo ameandika: I’m so happy I reached 100 million friends on Facebook. It’s amazing! Thank you everyone.

Friday, October 10, 2014

Spain yapoteza mechi ya kwanza ya kufuzu Euro 2016 baada ya miaka 8.

s48

Timu ya taifa ya Hispania jana usiku ikiwa ugenini ikicheza mchezo wao kugombea kufuzu Euro 2016 dhidi ya Slovakia, ilijikuta ikifungwa katika kipindi cha kwanza kwa makosa ya kipa Iker Casillas aliyefanya uzembe wa ajabu na kuruhusu Slovakia kupata goli la kuongoza kupitia free-kick iliyoenda moja kwa moja ndani ya nyavu.
Katika dakika 83, mchezaji wa Spain, Paco Alcacer alisawazisha na mashabiki wengi wakajua mchezo huo utaisha kwa sare lakini goli la mchezaji wa zamani wa Chelsea na Rangers, Miroslav Stoch likaipa Slovakia ushindi katika dakika 87 dhidi ya mabingwa watetezi wa Ulaya.
Baada ya mchezo huo wachambuzi wa soka wamesema sasa inabidi apewe nafasi David De Gea na Iker Casillas apumzishwe. Hii ni mechi ya kwanza kwa Spain kupoteza katika hatua ya kufuzu michuano ya Ulaya au kombe la dunia katika kipindi cha miaka 8. Diego Costa bado hajafanikiwa kuifungia Spain goli tangu alipoamua kuitumikia timu hiyo.

Monday, October 6, 2014

Picha: Arsene Wenger na Jose Mourinho walivyotaka kuzichapa uwanjani.

1412517546264_wps_25_Chelsea_V_Arsenal_5_10_20




Kocha wa Arsenal, Arsene Wenger na mwenzake wa Chelsea, Jose Mourinho almanusra wageuke Mayweather na Maidana kwenye mechi kali iliyofanyika Stamford Bridge kati ya timu hizo.
Wakati mechi ikiendelea ikiendela palitokea kutokuelewana baina ya makocha hao wawili baada ya Wenger kumfuata Mourinho na kuanza kusukumana baada ya beki wa Chelsea, Cahil kumchezea rafu Sanchez.
1412518009731_wps_32_Chelsea_s_Portuguese_mana
Mwamuzi akijaribu kuwaamua
Makocha hao walijikuta wakianza kusukumana na nakutokea mzozo hadi mwamuzi alipowafuata na kuwapa onyo kuwa wakiendelea atawatoa wote nje ndipo walipotulia. Mchezo uliisha kwa Chelsea kushinda 2-0.
Akiongea na waandishi wa habari, Wenger alisema hajutii kitendo hicho.
1412518223101_Image_galleryImage_LONDON_ENGLAND_OCTOBER_05
Mzozo huo uliteka hisia za watu wengi
1412517666924_wps_30_Arsene_Wenger_manager_hea
Ubabe ubabe tu
1412517665657_Image_galleryImage_Arsene_Wenger_manager_hea

Wednesday, October 1, 2014

Video: Angalia Ronaldo Wa Bandia Anavyotamba Mitaani.

Video: Angalia Ronaldo Wa Bandia Anavyotamba Mitaani
Akionekana ni mwenye ngozi nyororo na umbo lenye mvuto kama mshambuliaji wa klabu bingwa barani Ulaya Real Madrid, kijana anaetambulika kwa jina Joe Weller, amekua akiwahadaa wasichana kwa kujifafanisha na Cristiano Ronaldo.
Kijana huyo amekuwa akifanya matukio ya kuwahadaa watu hususana wasichama, katika mji wa Brighton uliopo kusini mwa Uingereza ambapo mara kadhaa wasichana wamekua wakivutiwa nae na kufikia hatua ya kumtamani kutokana na mvuto wake.
 

Hata hivyo wasichama wengi wamekuwa wakiamini kijana huyo ndio Ronaldo wa ukweli, kutoka kwenye klabu ya Real Madrid kwa namna anavyovaa na muonekano wake na pia hutumia matamshi ya maneno ya lugha ya kireno.
Mbali na hivyo wasichama wengine hufika mbali zaidi kwa kutaka kumbusu na kumkumbatia ikiwa ni sehemu ya kutaka kuonyesha hisia zao kimapenzi kwa Cristoano Ronaldo ambaye inasemakana hupata wakati mgumu anapokutana na wakinadada mitaani.


Fabregas Na Filipe Luis Watupia Picha Za Shangwe la Ushindi Instagram.

Fabregas Na Filipe Luis Watupia Picha Za Shangwe la Ushindi Instagram

Kiungo kutoka nchini Hispania, Cesc Fabregas pamoja na beki wa pembeni kutoka nchini Brazil Filipe Luis wameanika picha za wachezaji wenzao wa klabu ya Chelsea katika mtandao wa kijamii wa Instagram kwa dhamira ya kuonyesha namna walivyokuwa na furaha mara baada ya kupata point tatu ugenini usiku wa kuamkia hii leo huko mjini Lisbon nchini Ureno.
Fabregas na Filipe Luis, walikuwa sehemu ya kikosi cha Chelsea kilichoibuka na ushindi katika mchezo huo dhidi ya Sporting Lisbon, wameweka picha katika mtandao huo zikionyesha matukio tofauti ya furaha.
Picha ya Filipe Luis inaonyesha furaha iliyokuwa imekithiri miongoni mwa wachezaji wa Chelsea walipokuwa katika vyumba vya kubadilishia na picha ya Fabregas inaonyesha wachezaji wa Chelsea kwenye ndege tayari kwa safari ya kurejea jijini London nchini Uingereza.
Katika mchezo huo Chelsea walifanikiwa kuchomoza na ushindi wa bao moja kwa sifuri lililofungwa na kiungo kutoka nchini Serbia, Nemanja Matic.

Arsene Wenger Ni kiboko ya Mameneja 207 Wa Ligi Ya England Kwa Miaka 18.

Arsene Wenger Ni kiboko ya Mameneja 207 Wa Ligi Ya England Kwa Miaka 18

Meneja wa klabu ya Arsenal, Arsene Wenger hii leo ametimiza miaka 18 kamili tangu alipoanza kuitumikia klabu hiyo ya kaskazini mwa jijini London oktoba mosi mwaka 1996.
Wenger, anatimiza miaka 18 huku hii leo kikosi chake kikikabiliwa na mchezo wa ligi ya mabingwa barani Ulaya dhidi ya Galatasaray kutoka nchini Urutuki ambapo itamlazimu kufanya jitihada za kuinogesha furaha ya kuwa klabuni hapo kwa muda mrefu kwa kikosi chake kusaka ushindi.
Uwepo wa meneja huyo kutoka nchini Ufaransa, unaendelea kumpa sifa ya tofauti katika ligi ya nchini Uingereza kutokana na kuwa mtu aliyedumu kibaruani kwa kipindi kirefu huku klabu nyingine zikifanya mabadiliko ya mara kwa mara katika mabenchi yao ya ufundi.
Tangu mwaka 1996 Arsene Wenger, akiwa meneja wa klabu ya Arsenal klabu nyingine 43 zilizoshiriki ligi tangu kipindi hicho zimebadilisha jumla ya mameneja 207 na kumuacha akiwa meneja pekee anaebaki kuwa kiongozi wa benchi la ufundi la The Gunners.
Kwa mantiki hiyo sasa Arsene Wenger, anaendelea kuwa meneja aliyedumu Arsenal kwa kipindi kirefu kuliko meneja mwingine yoyote aliyepita klabuni hapo na pia anakuwa meneja aliyekaa kwa kipindi kirefu zaidi ya wengine katika ligi ya nchini Uingereza baada ya kuondoka kwa Sir Alex Ferguson aliyekuwa akikinoa kikosi cha Man Utd.
Arsene Wenger alitambulishwa rasmi kuwa meneja wa klabu ya Arsenal Oktoba mosi mwaka 1996, baada ya kukamilisha mipangop ya kusaini mikataba na viongozi wa klabu hiyo Septemba 30 mwaka huo.

TEAM PARTICIPATING